Joseph Haule (amezaliwa tar.
29 Desemba1975) ni msanii wa
muziki wa hip hop kutoka nchini
Tanzania. Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama
Professor Jay.
Katika Tanzania, Prof. Jay anatazamika kama msanii aliyeweza kuwateka
wazee waweze kusikiliza muziki wa Bongo Flava. Hasa kwa kibao
alichofanya wakati yupo na kundi la Hard Blasters Crew –
Chemsha Bongo. Professor Jay anatokea kundi la
Hard Blasters Crew.
Kundi hili ni moja ya makundi yaliyofanya muziki huu ambao hujulikana
kama ‘muziki wa kizazi kipya’ kukubaliwa na sehemu kubwa ya wa
Tanzania.
Maisha ya muziki
Professor Jay alianza shughuli za muziki mnamo miaka ya 90 hivi na alijiunga na kundi la ‘
Hard Blasters Crew‘(HBC) mnamo mwaka
1994. Mwaka
1995 Jay na HBC walishinda kuwa kundi bora la Hip Hop nchini
Tanzania. Jay na HBC walitoa albamu ya kwanza iitwayo ‘Funaga Kazi’ mwaka
2000 Albamu hiyo inaaminika kwamba ilileta mapinduzi makubwa sana ya muziki wa Hip Hop nchini
Tanzania. Albamu hii yenye ujumbe mzito ina nyimbo kama ‘Chemsha Bongo’ na ‘Mamsapu’ ambazo zilichangia kufanya muziki wa ‘
Bongo Flava‘ kuwa wa kila rika na kupewa heshima. Kabla ya hapo muziki huu ulionekana kuwa ni muziki wa wahuni
Msanii Binafsi
Professor Jay aliamua kuwa msanii binafsi mnamo
2001
na muda mfupi baada ya hapo akatoa albamu yake ya kwanza iitwayo
“Machozi Jasho na Damu”. Albamu hii ilivuma haraka sana na kumfanya
Prof. Jay kupata tuzo ya kuwa mtunzi bora wa Hip Hop nchini Tanzania kwa
nyimbo yake ya ‘Ndio Mzee’ kutoka kwenye albamu hiyo. na ikifuatiwa na
Nyimbo ya “Piga Makofi na Bongo
Dar es Salaam“
Mwaka 2003 Alitoa albamu ya pili iitwayo “Mapinduzi Halisi” ambayo nayo ilishinda tuzo ya
Kili Music Awards kuwa albamu bora ya
Muziki wa Hip Hop nchini
Tanzania kwa
mwaka 2003. Albamu hii imebebanNyimbo kama “Zali la Mentali”, “Msinitenge,” na “Promota Anabeep”
Mpya imewahi
kuteuliwa kuwa ni albamu bora ya Hip Hop ,
Mtunzi bora wa nyimbo za Hip Hop, na
Nyimbo bora ya Hip Hop ya mwaka kwenye Kili Music Awards.
2006.”Nikusaidieje”. na Baadae
Kisima Music Awards ya
Kenya ilikuwa Nyimbo bora ya Hip Hop na Video bora ya Hip Hop kutoka nchini
Tanzania.
Albamu
Tuzo Alizopata
Wasanii alioshirikiana nao kimuziki
Lady Jay Dee. (
Bongo Dar es Salaam na Nimeamini)
Mc Babu Ayubu. ( Ndio Mzee )
Juma Nature. ( Ndio Mzee na Zali la Mentali )
Q Chilah. ( Msinitenge )
Inspector Haroun. ( Hakuna Noma )
Simple X. ( Piga Makofi na Hakuna Noma )
Jose Chameleone. ( Ndivyo Sivyo – Kutoka
Uganda )
Adili a.k.a Hisabati
Mwana FA (ni jukumu letu)
Albert magweir (Una)
Lady Jay Dee (Bongo Dar es Salaam & Niamini )
Mr II sugu (Inatosha)
Ngoni (Mapinduzi)
Jay Mo (Tathimini)
Ferooz (Zubeda)
Mkoloni (Promota anibeep) nk.
Diamond Plutnum (Kipi sijasikia)